Ngonjera Kuhusu Dini
1YAKOBO
Yesu Kristo ni mwanawe, muumba ye Rahamani
Hutambuhi i dadawe, maninga ‘ko fumbuani
Hadi lini sa takawe, ukweli kuambiweni
Dini sio hoja kamwe, aabudiwe Rabuka.
FATUMA
Yesu huyo si mwanawe, acha kunihadaani
Sikiza ndo uambiwe, nta toa sikioni
Uongo umejazawe, ndiposa hutambuani
Dini sio hoja kamwe, aabudiwe Rabuka.
2YAKOBO
Hijabu kavaa wewe, gurunedi wafichani
Na kanzu zizingatiwe, bastola zabebeani
Lolote baya na liwe, nyie ndio watendani
Dini sio hoja kamwe, aabudiwe Rabuka.
FATUMA
Mpumbavu na usiwe, hatufichi hata pini
Kanzu niza zamaniwe, tena walahi dhamani
Lolote tusingiziwe, wema sisi kutendani
Dini sio hoja kamwe, aabudiwe Rabuka.
3YAKOBO
Sauti na mpaziwe, Osama Bin vitendoni
Mbona sisi tuuliwe, na wenye uhayawani
Nyote mfuatiliwe, hadi yote mashimoni
Dini sio hoja kamwe, aabudiwe Rabuka.
FATUMA
Jioni tuadhiniwe, Yakobo wajichoshani
Magaidi na wenziwe, wote sio wenzetuni
Walahi hadi mwishowe, watachoka tafuteni
Dini sio hoja kamwe, aabudiwe Rabuka.
4YAKOBO
Twapagawa na kiwewe, nyie mwatutishiani
Uislamu upigiwe, na mifano vitabuni
Hatutaki hao mwewe, waua bila hilani
Dini sio hoja kamwe, aabudiwe Rabuka.
FATUMA
Mkuki chungu kwa nguruwe, vurugu nazuiani
Dini ni yako huruwe, yaache ya mifanoni,
Duniani kuguriwe, ndo kuishi kina nani?
Dini sio hoja kamwe, aabudiwe Rabuka.
5YAKOBO
Nakubaliana nawe, meanza ona kanani
Mimi tangu nizaliwe, sijajua ukwelini,
Habari zinyunyiziwe, kwa wengine asilani
Dini sio hoja kamwe, aabudiwe Rabuka.
FATUMA
Dini na zifurahiwe, silete vizingitini
Umoja na uenziwe, hadi watoka hindini
Kwa kweli tusiletewe, ya makuu kuvunjani
Dini sio hoja kamwe, aabudiwe Rabuka.
Kakaa.. Huishi kunisisimua
Zuri sana hili.. Dini sio hoja kamwe kwa kweli
LikeLiked by 1 person
Sisi ni binadamu wa kawaida, dini si hoja kamwe ya kutufanya sisi tujigawanye. Tuishi pamoja kama ndugu.
LikeLike