Uncategorized

KUJAMIIANA. 

Kuwa mume ama mke, Rabuka katujalia                                                 Na mipango teketeke, yeye katuandalia                                         Kamwe usiiteleke, aliyokuchagulia                                                   Yarabi Mola twokoe, Dunia imepasuka.

Mume na aoe mke, Rabuka katuamrisha
Ila mke yu na mke, kitendo cha kupotosha
Aibu kwa toto jike, kwa anayowasilisha

Yarabi Mola twokoe, Dunia imepasuka.

Ndume naye sisazike, kwa yake kuabisha
Ushoga na usitike, da! tabia yapotosha
Wavyele wawajibike nyendo hii yapotosha

Yarabi Mola twokoe, Dunia imepasuka.

Jamii na igutuke, mema tuishi maisha
Kiona mui sivuke, letu kumrekebisha
Wala simpige teke, lengo letu kuboresha

Yarabi Mola twokoe, Dunia imepasuka.

Stephen Mburu
Malenga wa michepuko

4 thoughts on “KUJAMIIANA. ”

Leave a reply to Felix Achola Odhiambo Cancel reply